Tuesday, April 23, 2013

THE WORLD OF WONDERS "UPSIDE DOWN HOUSES" AU "NYUMBA ZILIZOJENGWA JUUCHINI"

hizi ni picha ya nyumba ambazo zimejengwa kwa muonekano tofauti kwamba zinatazama chini kwa maana muonekano wake ni kama paa la nyumba lipo chini
TAZAMA NYUMBA HIZI UJIONEE MWENYEWE

http://cdn.freshome.com/wp-content/uploads/2007/09/upside-down-house2.jpg.

 http://blog.petaflop.de/wp-content/uploads/2007/12/wonderworks-upside-down-house-haus-auf-dem-kopf-smoky-mountains-pigeon-forge-tennessee-tn-usa.jpg.

 http://i.telegraph.co.uk/multimedia/archive/00801/upside-down-house_801556i.jpg.
\
 http://resources0.news.com.au/images/2010/03/16/1225841/270284-upside-down-house.jpg.
 huu ndo muonekano wa ndani

 http://farm5.staticflickr.com/4078/4778823567_62d3c7a4aa_z.jpg.

 http://www.ripleys.com/weird/files/2012/05/UpsideDownHouse5.jpg.

 http://cdn0.lostateminor.com/wp-content/uploads/2012/05/UpsideDownHome2.jpg.

 http://1.bp.blogspot.com/-RnT9gr1Xs_k/T7e1-huU22I/AAAAAAAAKDQ/dL0cmt70euI/s1600/upside-down-house-sabah.JPG

Saturday, April 20, 2013

LIL WAYNE "TUNECHI" IN TROUBLE

http://assets.nydailynews.com/polopoly_fs/1.172064.1314040956!/img/httpImage/image.jpg_gen/derivatives/landscape_635/alg-court-lilwayne-jpg.jpg It has been reported that legendary producer, Quincy Jones and his lawyers have filed papers to have Lil Wayne’s multi-million dollar mansion and Bugatti Veyron car seized in order to settle a lawsuit again the rapper.

Quincy Jones filed a counter-suit against Lil Wayne for US$3.4 million after Lil Wayne himself filed a lawsuit against Jones. Weezy’s lawsuit stemmed from a documentary about the rapper that chronicled his addiction to Codeine. The rapper then made an effort to quiet the documentary’s release. Jones’ suit is against Lil Wayne for sabotaging the marketing of the documentary.

Lil Wayne’s camp however denies these claims and states that Lil Wayne will have no issues settling the matter before his property and assets are seized.

MAKAHABA WAWAVALIA NJUGA POLISI

http://1.bp.blogspot.com/--rWzm9iVdsE/UIc-gPL6IMI/AAAAAAAABT0/uW-W06MAnKU/s1600/MALAYA+WA+DAR.jpg
Jeshi la Polisi mkoa wa kipolisi Kinondoni, limelalamikiwa kwa vitendo vya baadhi ya askari wake kuvamia vyumba vinavyodaiwa kupangwa na watu wanaodaiwa kuwa makahaba (madanguro) na kuwapora fedha, simu na vitu vingine vya thamani nyakati za usiku.

Aidha, askari hao wamedaiwa kuwageuza wanawake hao mashine za kutolea fedha (Atm) ambapo hufika katika vyumba vyao kila baada ya wiki moja na kuwadai fedha kati ya Sh.30,000 na 50,000 kila mmoja kama hongo ili wasiwafikishe polisi.

Malalamiko hayo yametolewa na baadhi ya akina mama wanaoishi eneo la Mwananyamala walipozungumza na NIPASHE baada ya askari hao kukamata wanawake zaidi ya 87.
Kiongozi wa wanawake hao, Judith Rugamwa alidai kuwa, askari hao kutoka vituo vya Oysterbay na Mabatini wamekuwa wakiwanyanyasa kwa kuwapiga, jambo ambalo ni kinyume cha haki zao binadamu.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhZYTxnUCJG-rae7vhZYLv1sVQFY-yg1aHPlIWVhq7KUhqX8XvJ62bW8qFZAVkKHx2sQOz7NeU4DO4W-G30u2JMLcWcrDqVoP-4l-TN3n5CteAFfJP8uFylCxZIJ-gQixdim__JPk0qye8/s1600/African.jpg
"Wakitukamata huwa wanasema kosa letu ni kufanya ukahaba, lakini tukifikishwa kortini kosa linabadilika na kuwa uzembe na uzururaji, wakati wametukamata vyumbani kwetu ," alisema Judith.

Alisema wamechoka kunyanyaswa kama wakimbizi na kuonya kuwa sasa wanajiandaa kupambana na kila askari atakayefika hasa nyakati za usiku na kuwavunjia milango ya vyumba vyao ili kuwamata na kuwalazimisha wawape fedha huku wakimtaja afande Swai na Emma kuwa ndiyo wanaoongoza uovu huo.
Akizungumzia tuhuma hizo, afande Swai alijitetea kuwa yeye binafsi hajawahi kushiriki katika kuomba fedha wala kupora simu za wanawake hao licha ya kukiri kuwa ndiye anayeongoza misako yote Kinondoni.

"Kuhusu madai ya kuomba fedha, siwezi kukataa kwa sababu mimi huwa siingii vyumbani kukamata wanawake hao, badala yake askari wangu ndiyo wanaohusika moja kwa moja kabla ya kuwaleta katika gari ambayo huwa nawasubiri, lakini kama wanafanyiwa hivyo naomba wawataje kwa majina askari hao," alisema.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhiAkn3MGj30zEYS5SeEWETKg4jrTyz4-WRCGQL0MA1Zb5cS1guySfjeQqAXv9tZUsw8UpLvceGABG7-w8x_vrXMk33ykcZhugxOQMz8srkmbBtpH0y3hdo2Oo2Prl49TmQA31D4ou2X3ob/s1600/MALAYA.jpg
Kwa upande wake Kamanda wa polisi mkoani wa Kinondoni (RPC), Charles Kenyela, alisema amri ya kuwasaka na kuwakamata makahaba hao huwa inatolewa na ofisi yake na kwamba madai ya polisi wake kuchukua fedha na simu za watuhumiwa ni uongo mkubwa.
"Kama kuna mtu amewahi kufanyiwa hivyo aje ofisi kwangu na ushahidi ili ofisi yangu ichukue hatua kali za kinidhamu kwa sababu anayeshawishi, anayetoa na kupokea rushwa wote wanafanya makosa, waache kulalamika waje niwasilikize," alisema Kenyela.

MAUAJI DAR, "MTU MMOJA AUAWA KIKATILI"


 kamanda wa polisi,mkoa wa kipolisi temeke engelbert kiondo

Mtu mmoja jijini Dar es Salaam ameuawa kinyama kwa kupigwa, kisha mwili wake kuingizwa ndani kiroba na kutupwa ndani ya mtaro wa maji. Mwili wa mtu huyo umeokotwa jana majira ya saa 2:00 asubuhi eneo la Nyamachoma Yombo Buza baada ya wakazi wa eneo hilo kusikia harufu kali kutoka kwenye mtaro wa maji machafu pembeni ya barabara ya Yombo.

Baadhi ya wananchi walioshuhudia tukio hilo, walisema mwili huo wa mtu mwanaume ulikutwa ukiwa umewekwa ndani ya viroba viwili, kisha kutupwa kwenye mtaro kama takataka na watu wasiojulikana. Mwanamke mmoja aliyejitambulisha kwa jina mama Hassani, alisema chanzo cha kugundulika ni harufu kali iliyokuwa ikitoka kwenye mfuko huo na kusambaa eneo lote. "Baada ya kusikia harufu, tulianza kusaka inatokea wapi, ndipo tulipogundua inatoka kwenye mzigo wa kiroba uliokuwa ndani ya mtaro wa maji," alisema mwanamke huyo.

 Alisema, kutokana na hali ya mzigo huo, walijua ndani yake kuna takataka, lakini walipoondoa kiroba hicho walikuta miguu ya mtu. Hata hivyo, walishindwa kuendelea kuondoa kiroba kingine na kuamua kuwaita polisi ili kwenda kuuchukua mwili huo. "Inaelekea mtu yule aliuawa siku tatu zilizopita nyakati za usiku, kwa sababu ndani ya kiroba alikuwa katika hali ya kuchuchumaa na mikono yake imefungwa kamba kwa nyuma," alisema mkazi mwingine Abubakar Saidi. Mashuhuda hao walisema askari polisi walifika eneo la tukio majira ya saa 4:30 asubuhi na kuuchukua mwili huo na kuupeleka kituo cha polisi Chang'ombe. Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Temeke, Engelbert Kiondo, alipoulizwa kuhusu tukio hilo, alisema bado hajapata taarifa kuwepo kwa tukio hilo.

Friday, April 12, 2013

NEW SONG "Nesta ft rich mavoko ~nyota (prod by; sheddy clever)" LISTEN HERE AND DOWNLOAD FROM HERE

WAANDISHI WAFARIKI KWENYE AJALI TANGA

waandishi watatu wafariki dunia wakiwa kwenye msafara wa Mkuu wa Wilaya ya Handeni, baada ya gari walilokuwa wakisafiria la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo kuacha njia na kupinduka.
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Muhingo Rweyemamu, alisema tukio hilo lilitokea jana saa 3:30 katika kijiji cha Misima wakati wakielekea katika kijiji cha Nzundu kwenye zoezi la upandaji miti lililokuwa likifanyika kiwilaya kijijini hapo.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjUegGFyV0PXZu8JMMc8FNZbiyg6WJPnUBaueX-SEhC3O14AXRdGNYEAI0uN2NKdXirbz_dVj8aoqEIEgfgSGIvMdvWehurD5lWUmJADssJrFcMlVRbdwoXW8vKbRTcrcBkjcKdzFaJbN0/s1600/Handeni+Tanga.PNG
Aliwataja waliofariki papo hapo baada ya ajali kutokea kuwa ni Hamis Bwanga ambaye ni mwandishi wa gazeti la Uhuru na Mzalendo na Ofisa Uhamiaji Wilaya ya Handeni, Mariamu Hassani.
 
Rweyemamu alisema mwandishi  Sonyo Mwankale (Hussein Semdoe), alifariki dunia akiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Handeni akipatiwa matibabu.
Katika ajali hiyo, Mwankale ambaye alijeruhiwa vibaya sehemu za kichwani, baada ya kupelekwa hospitalini hapo, Mkuu wa Wilaya ya Handeni alimuomba helkopita Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini (IGP) Said Mwema, kuwachukua majeruhi hao, lakini kabla haijafika mwandishi huyo akafariki dunia.
Wengine waliyojeruhiwa katika ajali hiyo na kulazwa kwenye hospitali hiyo ni Mshauri wa Mgambo Wilaya, Athanas Paulo, Ofisa Misitu Wilaya, Natorin Mloe na dereva wa gari hilo lenye namba za usajili STK 4673, Mlawa Makata.
 
Habari zilieleza kuwa chanzo cha ajali hiyo ni gari hiyo ya Mkurugenzi Mtendaji wa Wilaya ya Handeni, kupasuka gurudumu la nyuma na kuacha njia kisha kupinduka. Hata hivyo Mkurugenzi huyo hakuwamo katika gari hiyo.
Wakizungumzia ajali hiyo, kwenye eneo la tukio, mashuhuda hao alisema watu hao walipoteza maisha muda mfupi mara baada ya tukio hilo na kwamba wananchi waliyojitokeza kutoa msaada walishuhudia hali za majeruhi hao zikiwa mbaya.
 http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/66/Handeni.GIF/250px-Handeni.GIF
Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Rweyemamu akizungumzia tukio hilo alisema kifo cha Afisa Uhamiaji huyo ni pigo kwa wilayani kwani ni hivi karibuni alisaidia kukamatwa kwa wahamiaji haramu 74.
Ofisa misitu Wilaya ya Handeni, Mloe akizungumzia jinsi ajali hiyo ilivyotokea akiwa katika hospitali ya Wilaya Handeni alikolazwa, alisema wakiwa safarini mbele alijitokeza mwendesha pikipiki (bodaboda) akitaka kujaribu kuwapita.
 
Alisema dereva wa gari lililobeba alimkwepa dereva wa bodaboda na kusababisha gari kuyumba na kusababisha kupinduka upande wa pili wa barabara na hivyo kusababisha kifo cha Afisa Uhamiaji na mwandishi wa gazeti la Uhuru papo hapo.

Monday, April 08, 2013

NEW SONG; RICH MAVOKO "LABDA NISEME NA MOYO" DOWNLOAD AND LISTEN HERE

baada ya kuachia video ya wimbo wake wa "one time" na kuafanya vizuri katika soko la muziki huu ndo ujio mwngine wa rich mavoko na wimbo wake mpya unaoitwa "bora niseme na moyo" SIKILIZA NA DOWNLOAD WIMBO HUU HAPA....
.


Saturday, April 06, 2013

MTUHUMIWA WA MAUAJI YA PADRE MUSHI AFIKISHWA KORTINI

,,



Mtuhumiwa wa mauaji ya Padri Evarist Mushi wa kanisa la Roman Katoliki jimbo la Zanzibar, Omar Mussa Makame (35), jana amefikishwa mahakamani kusomewa shitaka lake.
 
Mtuhumiwa huyo ambaye aliwahi kuwa mgombea wa nafasi ya Uwakilishi katika jimbo la Raha Leo kwa tiketi ya Chama cha Wananchi (CUF), anatuhumiwa kufanya mauaji hayo Febuari 17, mwaka huu.
 
Alifikishwa mahakamani majira ya saa 5 asubuhi na kusomewa mashtaka na Mwanasheria wa Serikali kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar (DPP), Abdallah Issa Mgongo, akisaidiwa na Mohamed Saleh Iddi.
 
Alidai kuwa Febuari 17, mwaka huu majira ya saa 12:59 asubuhi, mshitakiwa anatuhumiwa kumuua Padri Mushi kinyume na kifungu cha 196 na 197 cha sheria namba ya 6 ya mwenendo wa makosa ya jinai ya mwaka 2004.
 
“Mshtakiwa anatuhumiwa kumuua Padri Mushi, katika eneo la Beitrasi, majira ya saa 12:59 kinyume na sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai ya Zanzibar,” alisema Mgongo.
 
Hata hivyo, Mgongo alisema upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamilika na kuiomba mahakama kupanga tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo ambayo inasikilizwa na Jaji wa Mahakama Kuu, Mkusa Isaack Sepetu.
 
Kwa upande wake, baada ya kusomewa shtaka hilo, Omar Mussa Makame alikana kosa hilo na anatetewa na Wakili Abdallah Juma Mohamed akisaidiwa na Rajab Abdallah Rajab.
 
Kabla ya mtuhumiwa kusomewa shtaka lake, Wakili Abdallah Juma alioomba mahakama itoe mwongozo kufuatia ombi alilofungua Mahakama Kuu, akitaka Naibu Mkurugenzi wa upelelezi na makosa ya jinai Zanzibar, aitwe mahakamani kueleza kwanini mteja wake hakufikishwa mahakamani tangu alipokamatwa Machi 17, mwaka huu, kinyume na sheria.
 
Alisema ombi hilo tayari limepangiwa kusikilizwa Aprili 8, mwaka huu, na ana wasiwasi kitendo cha mshtakiwa kufikishwa mahakamani na kusomewa shtaka lake kunaweza kuathiri mwenendo mzima wa ombi hilo na kuomba mahakama kuondoa shauri hilo la mteja wake kusomewa mashataka hadi hapo ombi lake litakapotolewa maamuzi.
 
“Ombi letu kwako mheshimiwa, naomba mahakama kuondoa shauri la kumsomea shtaka mtuhumiwa, ili kutoa nafasi ya kusikiliza ombi tulilolifungua mbele ya mahakama yako,” alisema Abdallah Juma.
 
Hata hivyo, mwendesha mashtaka wa serikali, Mgongo, alisema ombi hilo halina uhusiano na Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka, na wala haijataarifiwa kuhusu kufunguliwa kwa ombi la kuhusiana na kesi hiyo.
 
“Ofisi ya DPP haijataarifiwa kuhusu ombi hilo, na haina taarifa yoyote, na kwa mujibu wa katiba, Mkurugenzi wa Mashtaka ndiye mwenye mamlaka ya kufungua kesi na ndicho kilichotuleta hapa,” alisema Mgongo.
 
Aidha alisema ombi lililofunguliwa mahakamani haliathiri shauri liliopo mbele na kuitaka mahakama kuzingatia kilicholetwa mbele yake, nacho ni kumsomea shtaka mtuhumiwa wa mauaji hayo.
 
Kwa upande wake, Jaji Mkusa baada ya kusikiliza pande hizo mbili, alisema kwamba ombi lililofunguliwa katika mahakama na wakili wa mtuhumiwa, la kuhoji kwanini hakufikishwa mahakamani ndani ya saa 24, bado haliathiri hatua ya kumsomea shtaka mtuhumiwa.
Jaji Mkusa alisema ombi lililofunguliwa litaendelea kusikilizwa kama lilivyopangwa, na mahakama, kazi yake kubwa ni kutafsiri sheria na kuhakikisha haki inatendeka kwa mujibu wa sheria.
 
Hata hivyo, Jaji Mkusa alitoa angalizo kwa vyombo vya habari kuwa makini wanaporipoti kesi ya mauaji kama hiyo, ili kuepuka kuvaa koti la mahakama la kumhukumu mtu kabla ya kuhukumiwa na mahakama ambayo ndio yenye jukumu hilo kwa mujibu wa katiba ya nchi.
Jaji Mkusa ameiahirisha kesi hiyo hadi Aprili 18, mwaka huu.
Padri Evarist Mushi aliuawa kwa kupigwa risasi wakati akienda kuongoza misa ya Jumapili, katika kanisa la Mtakatifu Theresia lililopo eneo la Beitrasi, nje kidogo ya Mji wa Zanzibar.