Wednesday, June 26, 2013

BOB JUNIOUR AKIPOKEA KICHAPO CHA MWIZI BAADA YA KUIBA

.

 .

 ..

 Bob Junior ameshare picha hizi kwenye ukurasa wake wa Facebook na kuandika: Kwa Dizaini hii lazima nirudi kwetu K………..Aaaaah Maisha Haya Ya Bongo?,,,

SUGU AKAMATWA KWA KUMTUKANA WAZIRI MKUU PINDA

.

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ''Sugu" (Chadema), alikamatwa na polisi mjini hapa jana na kuhojiwa kwa saa mbili na nusu, akidaiwa kumtukana Waziri Mkuu Mizengo Pinda kupitia mtandao wa jamii wa ‘facebook’. Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime, alisema Sugu alikamatwa saa 8.00 mchana akitokea bungeni na kufikishwa katika Kituo cha Polisi cha kati kwa mahojiano.

Misime alisema polisi waliamua kumkamata mbunge huyo baada ya kugundulika kuandika maneno ya kumtukana Waziri Mkuu juu ya utendaji wake.

Mbunge huyo anadaiwa kumtukana Waziri Mkuu kufuatia kauli yake aliyoitoa hivi karibuni bungeni, katika kipindi cha maswali ya papo kwa papo.

Katika kauli yake hiyo, Pinda alivitaka vyombo vya dola ikiwemo Jeshi la Polisi kutowavumilia watu wanaotishia amani na utulivu hapa nchini.

"Ni kweli tulimkamata Sugu majira ya saa nane mchana na alihojiwa kuhusiana na tuhuma hizo, lakini alidhaminiwa na Tundu Lissu akiwa na mwalimu mmoja wa Sekondari ya Viwandani majira ya saa 10.30 jioni," alisema Misime.

"Hata hivyo mbunge huyo analazimika kufika tena kesho (leo) saa tatu asubuhi, kwa ajili ya kuendelea na mahojiano zaidi kuhusiana na kauli yake katika mtandao huo" alisisitiza Misime.

"Kwa leo (jana), tumekamilisha taratibu zetu ila tutaendelea kwa hatua zaidi kesho (leo), mara atakapofika kwani anatakiwa kufika asubuhi kesho," alisema Misime.

Mkuu huyo wa Jeshi la Polisi mkoani hapa, alisema Polisi itaendelea kumchukulia hatua zaidi kadiri itakavyoona inafaa, ikiwemo kumpeleka katika vyombo vya sheria.

Kamanda alisema Polisi haitasita kumkamata mtu yeyote ambaye ataonyesha kupandikiza mbegu za chuki ambazo zinaweza kuvunja amani na utulivu wa nchi na kuwataka watumiaji wa mitandao hiyo kuitumia kwa minajiri iliyokusudiwa na si kutukana.

Hivi karibuni kumezuka tabia ya baadhi ya wanasiasa kutumia mitandao ya kijamii kuwachafua watu mbalimbali, wakiwemo viongozi wa serikali kwa manufaa yao.

Kauli ambazo zimekuwa zikiandikwa na kuwekwa katika mitandao hiyo, zimekuwa zikijenga chuki kati ya wananchi na serikali yao ikiwemo viongozi.

AFRICA KUSINI YAJIANDAA NA KIFO CHA MANDELA

Thumbnail for 2119 

*Familia yake yakutana kwa dharura kijijini Qunu
*Yatembelea makaburi ya ukoo, wageni wazuiwa

SASA kuna kila dalili kuwa taifa la Afrika Kusini, limeanza kujiandaa kukabiliana na tukio zito la kifo cha Rais wa Kwanza wa Taifa hilo, Nelson Mandela (94), ambaye amelazwa kwa siku 18 hospitalini akisumbuliwa na maradhi ya mapafu. Kauli tofauti kuhusiana na mwenendo wa hali ya afya yake na matukio mbalimbali yasiyokuwa ya kawaida yanayoripotiwa kufanywa na familia yake, ndiyo ambayo yameamsha hisia hizo.
Taarifa zilizopatikana jana kutoka nchini Afrika Kusini, zinaeleza kuwa watu muhimu katika familia ya Mandela, walikutana kwa dharura na kufanya mazungumzo ya faragha katika kijiji alichozaliwa cha Qunu.

Wakati wanafamilia hao wakikutana, msafara wa magari ya kundi jingine la wanafamilia, ulitembelea eneo la makaburi ya ukoo wa Mandela.

Eneo hilo la makaburi ya ukoo lipo mita chache kutoka yalipo makazi ya mdogo wake, Morris Mandela, mkabala na nyumba ya Mandela iliyoko kijijini Qunu.

Haikufahamika mara moja mazungumzo ya wanafamilia yalihusu jambo gani, lakini baadhi ya vyombo vya habari vya Afrika Kusini, vililiripoti kuwa kwa mujibu wa mila na desturi za kabila la Xhosa, wanafamilia hutembelea eneo la maziko iwapo kuna hisia za mmoja wa wanafamilia kufariki dunia na wakati mwingine kufanya tambiko la kimila.

Waliofika eneo la makaburi ni Winnie Madikizela-Mandela ambaye ni mke wa zamani wa Mandela, Waziri wa Utumishi wa Umma, Lindiwe Sisulu na Kiongozi wa chama cha upinzani cha United Democratic Movement, Bantu Holomisa.

Msafara wao ulifika eneo la makaburi jana asubuhi na kulikuwa na taarifa kuwa mtoto wa kike wa Mandela, Makaziwe Mandela, aliitwa eneo hilo.

Waandishi wa habari walizuiliwa kuvuka geti la eneo la makaburi hayo na waliofika nyumbani kwake Qubu, walipigwa marufuku kusogea karibu na nyumba hiyo.

Wanafamilia walioripotiwa kukutana kijijini Qunu ni Mandla Mandela, Thanduxolo Mandela, Ndaba Mandela na Ndileka Mandela na Chifu Bhovulengwe wa Baraza la AbaThembu.

Kikao hicho kinaeleza kuketi kuanzia saa nne asubuhi, lakini baadhi ya wanafamilia waliotakiwa kukihudhuria walichelewa kwa sababu ya kutopata taarifa mapema.

HII NDIO KAULI YA KAJALA BAADA KUSADIKIKA KUPIGWA CHINI NA WEMA

.


“Unajua mi nashangaa sana watu wanatoa wapi maneno wanayoandika, mimi sina tatizo na Wema, wala siwezi kuwa na tatizo naye, wema amekuwa msaada mkubwa kwangu, sa sijui nitagombana nini na wema, huo ni uzushi tuu jamani, muwe mnatuuliza kabla ya kuandika” Alisema kajala
Alipoulizwa kuhusu ukaribu wake mpya na wolper alisema
“Wolper nimekutana naye kwenye party ndo tukaamua kupiga picha, au siku hizi sitakiwi kupiga picha na mtu mwingine zaidi ya wema? Wolper ni rafiki yangu”

Saturday, June 01, 2013

KLYINN AWEKA WAZI UHUSIANO WAKE NA REGNALD MENGI

Ama kweli pesa na mapenzi kila kitu hebu sikia hii….
Kumekuwepo na Minong’ono mingi lakini hapakuwa na ushahidi wa hili mpaka mwanadada huyo alipoamua kuanika hadharani kuwa mheshimiwa Reginald Mengi ndiye baba halali wa mapacha wake wawili.
Hongera Mmiliki  wa makampuni ya IPP bwana REGINALD mengi kwa kumiliki mtoto mkali  Jackline Ntuyabaliwe(K’lyne)  ….


 MENGI.

 ..

 Hiyo ndo Tweet ya K’lyne kwa mpenzi wake Mh. MENGI