....
Jengo la ghorofa nne limeporomoka eneo la Kijitonyama wilaya ya
Kinondoni jijini Dar es Salaam jana na kusababisha kifo cha mtoto wa
miaka tisa na kujeruhi mmoja.
Tukio hilo lilitokea majira ya saa 10:45 jioni baada ya nguzo za jengo
hilo kutitia na kupelekea kuporomoka na hatimaye kusababisha kifo cha
mtoto aliyetambulika kwa jina la Joha Jeremia.
Juhudi za kuokoa zilifanywa na kikosi cha zimamoto ambao walifanikiwa
kumwokoa mfanyakazi wa nyumba hiyo aliyetambulika kwa jina la
Clementina Kipanjula (19).
Mwenyekiti wa mtaa wa Mpakani B kata ya Kijitonyama Barbo Kalinga
aliliambia NIPASHE kuwa ghorofa hilo lina zaidi ya miaka 20 na mmiliki
wake anaitwa Charles Lukumai ambaye alishafariki miaka mingi iliyopita.
Alisema katika ghorofa hilo kulikuwa na familia yenye mama na watoto wawili pamoja na mfanyakazi wa ndani waliokuwa wanaishi.
Omary Athumani ambaye ni mlinzi wa ghorofa hilo alisema alisikia mlio wa
kukatika kwa kitu lakini hakujua ni kitu gani, na ghafla akaona ghorofa
linadondoka.
No comments:
Post a Comment